TUKIO CHA KUPASULIWA KIFUA

Katika kipindi hiki ambacho Bwana Mtume alikuwa chini ya ulezi na uangalizi wa Bibi Haliymah alitokewa na tukio muhimu sana.

Hili lilikuwa ni tukio la kupasuliwa kifua chake na kutolewa fungu/uchafu wa shetani ili shetani asiwe na nafasi ya kumlaghai, kumshawishi na hatimaye kumpotosha.

Tukio hili lilikuwa kama ifuatavyo :

Mwenyezi Mungu alimpelekea Mtume wake wake naye akingali mtoto malaika wawili.

Wakati huo Mtume alikuwa akichunga mbuzi na kondoo pamoja na nduguze wa kunyonya (Watoto wa Bi Haliymah) jirani na makazi yao.

Malaika wale wakambeba Mtume wakamlaza chali na kumpasua kifua chake, wakautoa moyo wake na kuukosha.

Baada ya kuukosha wakaurudisha mahala pake na pale pale kifua kikawa kama kilivyokuwa mwanzo bila ya athari yeyote.

Yote haya yalitendeka mbele ya macho ya watoto wenzake, wakakimbia haraka kwenda kumueleza mama yao yaliyompata ndugu yao huyu.

Bibi Haliymah na mumewe wakatoka mbio kwenda kuangalia kulikoni, wakamkuta Mtume amesimama, wakamkumbatia na kumuuliza yaliyomsibu naye akawahadithia tukio zima lilivyojiri.

Wakamshukuru MwenyeziMungu kwa kumsalimisha salama lakini wakachelea yasije kumpata tena kama haya yaliyompata leo, hivyo wakaamua kumrudisha kwa mama yake.

 

TUKIO CHA KUPASULIWA KIFUA

Katika kipindi hiki ambacho Bwana Mtume alikuwa chini ya ulezi na uangalizi wa Bibi Haliymah alitokewa na tukio muhimu sana.

Hili lilikuwa ni tukio la kupasuliwa kifua chake na kutolewa fungu/uchafu wa shetani ili shetani asiwe na nafasi ya kumlaghai, kumshawishi na hatimaye kumpotosha.

Tukio hili lilikuwa kama ifuatavyo :

(more…)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *