TASHAHADU YA MWISHO {KATIKA KIKAO CHA MWISHO}

Ni wajibu kwa mwenye  kuswali akae  baada  ya sijda ya  mwisho ya swala yake asome “Tashahudi”  imepokelewa katika riwaya ya Ibn  Masoud Allah amuwiye radhi – amesema : Tulikuwa tukisema kabla ya kufaradhishwa juu yetu Tashahudi  

ASSALAAM ALALLAH KABLA IBADIHI, ASSALAAM ALAA JIBRILL, ASSALAAM ALA MIIKAIL, ASSALAAM ALA FULAN

Mtume   – Rehema na amani zimshukie  alipomalizaa kuswali alituelekkea , akatuambia “ Hakika  Allah ndiye AS – SALAAM , basi anapokaa mmoja wenu  katika   swala { Kwa  ajili ya Tashahudi } basi  na aseme  

ATTAHIYYAAT LILLAH WASSALAWATU WATTAYYIBAATU, ASSALAAM ALAYKA AYYUHA NNABII WARAHMATULLAH WABARAKATUH, ASSALAAM ALAYNA WA-ALAIBADILLAHI SSALIHINA

Kwani  nyinyi mtakapoisema {salamu  hii}  humpata {humfikia} kila mja mwema mbinguni na ardhini. Bukhaari na  Muslim.

Hili  ni mojawapo ya matamko  sahihi ya   Tashahudi ambayo  yaliyonukuliwa kutoka kwa Bwana  Mtume. Tashahudi yeyote iliyothibiti kutoka kwa Mtume mtu  akiisoma itamjuzia.

 

Sharti za Tashahudi.

Msomaji  wa Tashahudi analazimika kuchunga yafuatayo:

1.   Ajisikizishe  yeye  mwenyewe matamko ya Tashahudi  iwapo hana tatizo la kusikia.

2.   Kukifululiza kisomo cha tashahudi, yaani asiweke mwanya mkubwa baina ya ibara za Tashahudi . pia asitie kati dhikri nyingine , akifanya hivyo yaani akinyamaza kinyamao kirefu au  akilia kati dhikhri  nyingine , Tashhahudi yake  itakuwaa imebatilika na itamuwajibikia kuianza upya.  

3.  Aisome katika hali ya kukaa isipokuwa katika mazingira ya dharura tu ndio anaruhusiwa kuisoma  katika hali  yoyote imkinikiayo.

4.    Aisome kwa lugha ya Kiarabu . Akishindwa atasoma tafsiri yake kwa Lugha  yake, Lakini bado atakuwa na wajibu wakujifunza mpaka aweze kuisoma kiarabu kama alivyofanya Mtume wa Allah- Rehema na Amani zimfikie.  

5.  Achunge  matokeo ya herufi , shada na hukumu zote za usomaji . akifanya kosa lolote litakalopelekea  kuharibika  kwa maana,  halitamaanisha zaidi ya  kubahatilika Tashahudi yake  hiyo . Kwa  hivyo basi itamlazimu kuirejea upya .

6.  Ayatungamanishhe maneno ya Tashahudi  kwa mtungo wake kama yalivyopokelewa kutoka kwa Mtume wa Allah – Rehema na Amani  zimshukie .

 

 

TASHAHADU YA MWISHO {KATIKA KIKAO CHA MWISHO}

Ni wajibu kwa mwenye  kuswali akae  baada  ya sijda ya  mwisho ya swala yake asome “Tashahudi”  imepokelewa katika riwaya ya Ibn  Masoud Allah amuwiye radhi – amesema : Tulikuwa tukisema kabla ya kufaradhishwa juu yetu Tashahudi  

ASSALAAM ALALLAH KABLA IBADIHI, ASSALAAM ALAA JIBRILL, ASSALAAM ALA MIIKAIL, ASSALAAM ALA FULAN

Mtume   – Rehema na amani zimshukie  alipomalizaa kuswali alituelekkea , akatuambia “ Hakika  Allah ndiye AS – SALAAM , basi anapokaa mmoja wenu  katika   swala { Kwa  ajili ya Tashahudi } basi  na aseme  

(more…)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *