SWALI: Naomba kujuzwa, jina la Mtume wa Allah; Muhammad-Rehema na Amani zimshukie-limetajwa mara ngapi ndani ya Qur-ani Tukufu?
JIBU: Jina “Muhammad”-Rehema na Amani zimshukie-limetajwa mara nne ndani ya Qur-ani Tukufu, katika Sura zifuatazo:
- Surat Aali Imraan [03], aya 144: “Na Muhammad hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwishapita kabla yake Mitume…”.
- Surat Al-Ahzaab [33], aya 40: “Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu…”.
- Surat Muhammad [47], aya 2: “Na walio amini na wakatenda mema, na wakaamini aliyo teremshiwa Muhammad…”.
- Surat Al-fat-hi [48], aya 29: “Muhammad ni Mtume wa Allah. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya makafiri…”.
Kwa faida za muulizaji na wengineo, limetajwa jina “Ahmad” mara moja katika Surat Swaffi [61], aya 6: “Na Isa mwana wa Mariamu alipo sema: Enyi wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Allah kwenu, ninaye thibitisha yaliyo