SIJIDA MSOMO

Ni suna thabiti kutoka kwa Bwana  Mtume–Rehema na Amani zimshukie–kusujudu  sijida ya msomo. Suna hii inawahusu wote  wawili; msomaji wa Qur-ani na msikilizaji, iwe ni ndani ya  swala au nje ya swala.

 

I/.  SABABU YA  KUSUJUDU SIJIDA YA MSOMO:

Suna ya sijida ya msomo inapatikana kwa moja ya mambo mawili haya:-

1.  Kusoma aya ya Qur-ani ambayo ndani yake  kuna paliposuniwa kusujudu, au

2.  Kuisikia aya hiyo ikisomwa na mtu mwingine.

 

II/.  DALILI/USHAHIDI   WA SIJIDA YA MSOMO:

Kama tulivyokwishaeleza kwamba  sijida ya msomo ni suna iliyothibiti kutoka  kwa Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Na  ushahidi ni hadithi zifuatazo:-

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Umar–Allah awawiye radhi– amesema:

“Alikuwa Mtume wa Allah–Rehema  na Amani zimshukie –akitusomea sura ambayo ndani yake kuna sijida. Basi (hapo) husujudu nasi husujudu (pamoja  nae) kiasi  hata mmoja wetu hapati mahala pa kuliweka paji lake la uso (kutokana na  wingi wa watu)”.

Na katika riwaya iliyopokelewa na Abuu  Daawoud:

“Mtume– Rehema  na Amani  zimshukie-alikuwa akitusomea Qur-ani. Anapoipitia (aya ya) sijida  hukabiri na  kusujudu, nasi  tukasujudu pamoja nae”.

 

III/. FADHILA  ZA SIJIDA YA MSOMO:

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah-Allah amuwiye radhi-kutoka kwa Mtume wa Allah-Rehema  na Amani zimshukie–amesema:

“Mwanadamu ataposoma aya ya sijida na  akasujudu, shetani hujitenga na kulia akisema:  Ee ole wangu, mwanadamu ameamrishwa  kusujudu  akasujudu, basi yamuelea kupata    pepo ya  Allah.Nami  nimeamrishwa kusujudu  nikakhalifu amri ya (Mola  wangu ), basi nitaingia motoni”. Muslimu.

 

IV/. HUKUMU  YA  SIJIDA YA MSOMO:

Sijida ya msomo hukumu yake ni  suna ambapo mtu akisujudu hupata thawabu  na akiacha kusujudu hapati dhambi. Lakini  tu atakuwa amejidhulumu mwenyewe fursa  ya kujaza na kuithakilisha  mizani yake ya kheri. Dalili ya  haya ni hadithi zifuatazo:-

Imepokelewa  na Sayyidna Umar–Allah  amuwiye  radhi–amesema Mtume wa Allah–Rehema na  Amani zimshukie:

“Enyi watu hakika sisi (tunaposoma Qur-ani) tunazipitia aya  za sijida. Atakayesujudu (mahala  hapo) hakika atakuwa  amesibu (amepatia )  na asiyesujudu, basi hapana  dhambi juu yake”.  Bukhaariy

Na  imekuja katika riwaya ya Ibn Umar–Allah awawiye  radhi: 

“Hakika hakutufaradhishia  kusujudu ila tutakapo”.

 

V/. SHARTI ZA SIJIDA  YA MSOMO:

Sharti zilizoshurutizwa katika sijida ya msomo ni nafsi  ya  sharti  zilizoshurutiziwa swala. Sharti hizo  ni pamoja  na

twahara ya hadathi ndogo na kubwa.

Kuelekea Qiblah wakati wa   kusujudu, na

Kusitiri tupu.

Na baki ya sharti nyingine zilizotajwa katika kusihi kwa swala.

 

VI/. NAMNA  YA KUSUJUDU SIJIDA YA MSOMO.

Ni kusujudu  msomaji na msikilizaji wa Qur-ani anapoifia    aya  ya  sijida.

Kusujudu sijida moja iliyo baina ya takbira mbili,  takbira ya kuliweka paji la uso juu ya  ardhi  na  takbira ya  kuliinua kutoka hapo.

Kisha  hutoa salamu na wala hasomi Tashahudi. 

Imependelewa kwa mtu mwenye kusujudu sijida  ya msomo amuombe Allah kwa dua njema, hii  ni kwa sababu katika sijida ndipo mahala   mja huwa karibu zaidi na Mola  wake. Kwa mantiki hii na kujibiwa dua  akiomba pia huwa karibu zaidi mahala hapo kuliko mahala pengine.

 

VII/. MAHALA ZILIMO SIJIDA ZA MSOMO:

            Jumla ya sijida za msomo ndani ya Qur-ani  Tukufu ni kumi na tano kama ifuatavyo:-

SURA                            AYA

Al-a’araaf                          (7)  :206

Ar–ra’ad                           (13):15

An-nahl                           (16)  :49

Bani  Israil                        (17):107

Maryam                           (19)  :58

Al–Hajj                             (22):18

Al–Hajj                           (22):77

Al–Furqaan                     (25) :60

An–naml                          (27):25

As-sajdah                        (32):15

Swaad                             (38):24

Fuswilat                           (41):37       (Ha-Miym–sajdah)

An–najm                          (53):62

Al-inshqaaq                      (84):02

Al-alaq                             (96):19

 

 

SIJIDA MSOMO

Ni suna thabiti kutoka kwa Bwana  Mtume–Rehema na Amani zimshukie–kusujudu  sijida ya msomo. Suna hii inawahusu wote  wawili; msomaji wa Qur-ani na msikilizaji, iwe ni ndani ya  swala au nje ya swala.

I/.  SABABU YA  KUSUJUDU SIJIDA YA MSOMO:

Suna ya sijida ya msomo inapatikana kwa moja ya mambo mawili haya:-

1.  Kusoma aya ya Qur-ani ambayo ndani yake  kuna paliposuniwa kusujudu, au

2.  Kuisikia aya hiyo ikisomwa na mtu mwingine.

(more…)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *