SAFARI YA ISRAA

Mwaka   wa huzuni  ambamo Mtume  aliipoteza  mihimili  yake miwili; muhimili wa ndani, mkewe  Bi Khadijah  na Muhimili  wa nje Ami  yake Mzee Abuu  Twaalib;

Upasito wa   watu wa Makkah na mapokezi mabaya ya  watu  wa Twaif. Matukio  yote  haya  yalimtia  Mtume katika  hali ya huzuni  kuu, na kumkatisha  tamaa na watu  wake kwa kiasi kikubwa sana . 

Ni katika hali na mazingira haya ndipo Mwenyezi Mungu  Mtukufu  alipomkirimu  Mtume  wake safari  ya  Israa na Miiraji  kabla       ya Hijrah  ya Madinah.

Israa  ni ile safari  ya Bwana Mtume – Rehema  na Amani  zimshukie – kutoka mji mtukufu wa Makkah usiku mpaka  Baaytul-Maqdisi  Jerusalem,  Katika  nchi ya Palestine.

Ama Miiraji ni ile safari iliyoanzia   hapo  katika  Baytil-Muqaddas kuelekea ulimwengu  na anga  za juu kabisa (mbinguni)  kuonana na Mola wake na hatimaye  kupewa  zawadi  ya  swala  tano yeye na umati wake . 

Safari ya Israa imetajwa  ndani ya  Qur – ani   Tukufu: 

UTUKUFU  NI WAKE YEYE AMBAYE ALIMPELEKA  MJA WAKE USIKU (mmoja  tu) KUTOKA MSIKITI  MTUKUFU (wa makkah) mpaka MSIKITI WA  MBALI (wa Baytul-Muqaddas – Palestine) AMBAO (tumeubariki na) TUMEVIBARIKI VILIVYOKO  PEMBEZONI  MWAKE. (Tulimpeleka  Hivyo)  ILI TUMUONYESHE  BAADHI  YA   ALAMA  ZETU.  .HAKIKA  YEYE ( Allah)  M MWENYE KUSIKIA ( na )  mwenye kuona”  ( 17:1).

 Ama Safari  ya Miraji imepokelewa katika vitabu sahihi vya hadithi .

Hadithi  sahihi  zaidi katika kuitaja safari hii ni ile iliyopokelewa na kuitaja safari hii ni ile iliyopokelewa  na Maimamu  Bukhaariy  na Muslim na Kunakiliwa na Kadhi Iyaadh  katika kitabu chake kiitwacho “Shifaa”.

Imepokelewa riwaya kutoka  kwa swahaba wa Mtume : Anasi Ibn Maalik –  Allah amuwiye radhi –  amesema :

Amesema Mtume wa Mwenyezi  Mungu – Rehema  na Amani zimshukie ;  aliletwa buraqu, naye ni  mnyama  mkubwa kuliko punda na ni  mdogo chini ya  nyumbu.

(Spidi yake anapokimbia) huweka kwato zake ukomo wa macho yake”  Mtume akasema :

 Nikampanda  mpaka  nikafika  Baytul – Muqaddasi , Hapo nikamfunga kwenye  kikuku  ambacho  walikuwa wakimfungia Mitume (kabla yangu).

Kisha nikaingia msikitini na kuswali humo nakaa mbili  halafu  nikatoka ndipo Jibril aliponiletea chombo chenye  pombe na kingine  kina maziwa  (nichague)  nikachagua (na kunywa) maziwa. Jibril akasema umechagua jumbile (umbo).

Halafu tukapandishwaa mbinguni, Jibril akabisha hodi akaulizwa U nani wewe ?

Akajibu Jibril, akaulizwa (tena) U pamoja  na nani wewe ? Akajibu  Muhammad . Akaulizwa (tena) : Je ameitwa kuja  huku ? Akajibu , naam  ameitwa .

Tukafunguliwa , Kutahamaki huyu ndiye Adam, akanikaribisha na kuniombea dua njema. Kisha tukapandishwa mpaka uwingu wa pili, Jibril akabisha hodi  akaulizwa : U nani wewe?

 Akajibu Jibril, akaulizwa (tena) U pamoja  na nani wewe ? Akajibu  Muhammad. Akaulizwa ( tena ) ;Je  ameitwa kuja huku ?  akajibu naam ameitwa.

Tukafunguliwa tahamaki niko uso kwa uso na ndugu wawili wa mama mkubwa na mama mdogo ;  Yahyah na Issa mwana wa Mariam  Wakanikaribisha na kuniombea dua njema. 

Halafu Tukapandishwa uwingu wa tatu ( Jibril)  akataja ( maneno )  kama yale ya mwanzo basi  tukafunguliwa .

Kutahamaki huyu ndiye Yusuf naye akiwa  kapewa nusu ya uzuri akanikaribisha na kuniombea dua njema .

Kisha  tukapandishwa  mpaka uwingu wa nne , ( Jibril ) akataja ( maneno ) yale yale,  Tahamaki niko ana kwa ana  na Idrisa, akanikaribisha na kuniombea dua njema. Amesema Mwenyezi  Mungu Mtukufu katika Suurati Maryam.

 “NA  TULIMUINUA DARAJA YA JUU KABISA’  (19:57).

Kisha  tukapandishwa mpaka uwingu wa tano akataja maneno yale yale.

Tahamaki  niko mbele ya Haruni akanikaribisha na kuniombea dua njema .

Halafu tukapandishwa mpaka uwingu wa sita akataja maneno yale yale  Tahamaki huyu  ndiye  Musa akanikaribisha na kuniombea dua  njema.

Kisha tukapandishwa mpaka  uwingu wa saba  akataja maneno  yale yale.

Tahamaki niko  ana kwa ana na Ibrahim akiwa ameegemeza  mgogo wake kwenye (Msikiti wa) Baytul – Maamuri.

Msikiti huo huingiwa na malaika sabini alfu  (70,000)  kila siku (wapya  wasio wale waliopata kuingia).

Kisha ( Jibril) akanipeleka  mpaka penye Mkunazi wa kumalizikia ( mambo yote ) . Majani ya Mkunazi huo ni kama (Ukubwa wa) masikio ya tembo na matunda yake ni kama magurudumu. Mkunazi  ule ulipofunikwa  kwa amri ya Mola wangu , Ulibadilika.

Basi hakuna yeyote katika viumbe wa Mwenyezi  Mungu anayeweza kuusifia mkunazi huo kutokana na uzuri wake. Mwenyezi  Mungu akanifunulia hapo aliyonifunulia yaani wahyi na akanifaradhisha mimi na umati wangu swala  khamsini mchana na usiku.

Nikateremka   mpaka kwa Musa akaniuliza Mola wako ameufaradhishia nini umati wako ?  Nikamwambia swala Khamsini  akaniambia rejea kwa Mola ukamuombe akupunguzie kwa sababu umati wako hawataliweza hilo kwani mimi nimewajaribu Baniy Israil na kuwa na uzoefu nao. Akasema  (Mtume) Nikarudi kwa mola  wangu   na kumwambia ewe Mola  wangu  Wapunguzie umati wangu,  akanipunguzia Swala Tano (zikabakia  arobaini na tano).

Nikarejea  kwa  Musa nikamwambia amenipunguzia  tano. Akaniambia umati wako hawataziweza hizo, rudi tena kwa Mola wake ukamuombe akupunguzie;  Akasema (Mtume) 

“Nikawa nikienda na kurudi baina ya Mola wangu Mtukufu na Musa mpaka akasema utakatifu ni wake;  Ewe Muhammad  hizo ni swala tano kila mchana na usiku.  Kila swala moja kwa swala kumi basi hizo ni swala khamsini.  Na yeyote atakayekusudia kufanya jambo jema na asilitende, ataandikiwa jema moja,  Na atakayekusudia kutenda jema na akalitenda ataandikiwa mema kumi,  Na atakayekusudia kutenda na asilitende hataandikiwa chochote.  Na atakayekusudia kufanya ovu na akalifanya ataandikiwa dhambi/baya moja” 

Akasema Nikashuka mpaka kwa Mussa, nikampa khabari ya huko. 

Akasema rudi tena kwa Mola wako umuombe takhfifu nikamwambia nimerejea kwa Mola wangu mpaka nimeomuonea haya kisha Bwana Mtume – rehema na Amani zimshukie akarejea usiku ule ule kulipopambazuka akadamkia kwenye baraza ya Makurayshi.

Abu Jahli Ibn Hishaam akamjia nae akamuhadithia khabari yote iliyotokea Abu Jahli akaita Enyi Bany Ka’abi Ibn Luayyi njooni makafiri wa kikurayshi wakamjia, Bwana Mtume anaelezea khabari ile baada ya kuusikia wakawa wako miongoni mwao waliopiga makofi na wengine wakawa wameshika vichwa vyao kwa kustaajabu na kupinga.

Baadhi ya watu waliokuwa wamemuamini Mtume  waliritadi  na kurudi ukafirini, hawa walikuwa ni wale madhaifu na Imani. 

Baadhi ya watu wakamuendea rafiki mkubwa wa Mtume Bwana Abi Bakri na kumpasha khabari ile.  Akamwambia ikiwa amesema hivyo basi amesema kweli wakamwuliza  Unamsadiki kwa khabari hizi?  Akajaribu, Mimi ninamsadiki kwa khabari za mbali zaidi kuliko hizo (za kwenda Baytul-Muqaddasi usiku na kurudi hapa usiku huohuo).

Tangu siku hiyo ndipo alipoitwa Abu bakari Sidiyk (Abu Bakri Msadikrishaji). Kisha makafiri wale wakaanza kumtahini Mtume kwa kumuuliza sifa za msikiti  wa Baytul–muqaddasi na miongoni mwao walikuwepo walioujua. 

Ama Bwana mtume alikuwa hapata kuuona kabla ya safari hiyo. 

Mwenyezi Mungu akamletea Mtume wake msikiti ukawa mbele ya macho yake akawa anawasifia mlango baada ya mlango na sehemu baada ya sehemu. 

Wakasema ama kwa upande wa sifa tu amepatia kweli.  Sasa tuelezee khabari ya msafara yetu. Walikuwa na misafara yao ya biashara ikitokea shamu.  

Bwana Mtume akawaeleza idadi ya ngamia waliomo katika misafara hiyo na hali yake na akawaambia itakufikieni siku fulani mchana ikiongozwa na ngamia wa kijivu.  

Wakaondola wakiingojea siku hiyo kwa hamu,  akasema mmoja wao siku hiyo wallah Jua hilo limechomoza,  Na mwingine akasema Wallah na msafara huo umeingia na unaongozwa na ngamia wa kijivu kama alivyosema  Muhammad. 

Utabiri na ukweli huu wa bwana Mtume haukuwazidishia Mukurayshi ila kibri na upinzani mpaka wakasema huu ni uchawi wa dhahiri.

Asubuhi ya usiku ule wa safari ua Israaa na Miiraji, Jibril alikuja na akamfundisha Mtume jinsi ya kuswali na nyakati za swala. Aswali rakaa mbili alfajiri, rakaa nne adhuhuri na nyingine lasiri na rakaa tatu magharibi na nne ishaa. 

Bwana Mtume kabla ya kufaradhiwa suala alikuwa akiswali rakaa mbili asubuhi na jioni kama alivyokuwa  akiswali Nabii Ibrahimu – Rehema na Amani ziwashukie wote.

SAFARI YA ISRAA

Mwaka   wa huzuni  ambamo Mtume  aliipoteza  mihimili  yake miwili; muhimili wa ndani, mkewe  Bi Khadijah  na Muhimili  wa nje Ami  yake Mzee Abuu  Twaalib;

Upasito wa   watu wa Makkah na mapokezi mabaya ya  watu  wa Twaif. Matukio  yote  haya  yalimtia  Mtume katika  hali ya huzuni  kuu, na kumkatisha  tamaa na watu  wake kwa kiasi kikubwa sana . 

Ni katika hali na mazingira haya ndipo Mwenyezi Mungu  Mtukufu  alipomkirimu  Mtume  wake safari  ya  Israa na Miiraji  kabla  ya Hijrah  ya Madinah.

(more…)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *