SABABU ZA SIJIDA SAHW NA NAMNA YA KUISUJUDU

SABABU ZA  SIJIDA YA KUSAHAU:

Mambo yafuatayo ndio yatakayo mpelekea mwenye kuswali  kuleta sijida ya  kusahau:

1. Mwenye kuswali kuacha  mojawapo  miongoni  mwa suna za swala zinazoitwa “Ab-aadh”, mithili ya Tashahudi ya mwanzo na Qunuut  (kwa ufafanuzi wa kina juu ya suna hizi, rejea SURA YA PILI, SOMO LA KWANZA, SWALA {x} Suna za swala).

Imepokewa kutoka kwa Abdullah Ibn Buhaynah-Allah amuwiye radhi–kwamba yeye amesema:  Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-alituswalisha rakaa mbili za  swala fulani.

Na katika upokezi mwingine: “Aliinuka  kutoka katika  rakaa mbili za  swala ya Adhuhuri, kisha akasimama na  wala hakukaa (Tashahudi  ya mwanzo), watu (maamuma)  nao wakainuka pamoja nae. Alipomaliza swala yake  (kwa kuswali rakaa mbili za mwisho), (wakati) tukiingojea salamu yake,  akakabiri  (akasema  Allahu  Akbar) kabla ya kutoa salamu. Akasujudu  sijida mbili na il-hali amekaa,  kisha (ndio) akatoa salamu.” Bukhaariy &  Muslim.

Imepokelewa  kutoka kwa Al-Mughiyrah Ibn  Shu’ubah–Allah amuwiye radhi–amesema: Amesema Mtume wa Allah–Rehema na Amani  zimshukie:

“Atapoinuka mmoja wenu kutoka  (katika) rakaa mbili        (za mwanzo) na  akawa hajatimia hali ya  kusimama , basi na akae (kwa   ajili ya Tashahudi ya mwanzo. Na atapotimia  hali ya kusimama, basi na asikae (aendelee na  swala yake)  na atasujudu sijida mbili  za  kusahau”.Ibn  Maajah, Abuu Daawoud & wengineo.

 

2. Mtu kuwa na shaka ya  idadi ya rakaa alizoziswali. Katika hali hii, mwenye shaka anatakiwa aishike idadi ya chini na atimize rakaa  zilizobakia.

 Kisha  atasujudu  sijida ya kusahau  kwa ajili ya kuunga imkani ya kwamba yeye  amezidisha kitu katika swala yake.

Lau mtu  atakuwa  na  shaka je,  ameswali  Adhuhuri rakaa  tatu au nne? Shaka hii ikamtokea akiwa  bado ndani  ya swala, basi atachukulia kuwa  ameswali rakaa tatu na aongeze rakaa moja  nyingine ili zitimie rakaa nne zitakiwazo.

Halafu  tena  akimaliza asujudu sijida mbili za kusahau  kutokana na imkani ya kuwa kaswali  rakaa  tano na hivyo kuwa amezidisha  kitu katika  swala yake.

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Said–Allah   amuwiye radhi–amesema: Amesema Mtume wa  Allah–Rehema na Amani zimshukie:

“Atapotia  shaka  mmoja wenu ndani ya swala yake,  na asijue ameswali rakaa ngapi, tatu au nne? Basi (cha  kufanya) ni kuitupa  shaka hiyo na ajengee  alicho na yakini  nacho. Kisha asujudu sijida mbili kabla  ya kutoa salamu.  Akiwa ameswali  rakaa tano, (kusujudu huko)  kutaifanya   swala  yake  kuwa jozi  (ya  rakaa   mbili za  mwanzo  na mbili za  mwisho).  Na   akiwa ameswali    kutimiza rakaa nne, zitakuwa  (sijida  mbili) hizo zimemdhalilisha na  kumghadhibisha shetani”. Muslim.

Ama lau mtu alitia shaka   nje  ya swala  (baada ya kutoka  ndani ya swala) kwa yakini shaka yake hii  haitaathiri usahihi na ukamilifu wa swala  yake. Ila kama shaka hiyo itakuwa ni   katika nia na  Takbira ya kuhirimia swala,  shaka hii itamlazimisha  kuirudia (kuiswali  tena) swala yake.

 

TANBIHI:

Kusahau kwa maamuma wakati wa kumfuata Imamu wake, kama vile kusahau Tashahudi ya  mwanzo.

Kusahau kwake huku kutachukuliwa na Imamu wake na wala haitamlazimu kusujudu sijida mbili za kusahu baada ya  salamu ya Imamu wake.

Dalili ya  haya ni kauli   yake    Bwana  Mtume–Rehema na Amani zimshukie: “Imamu ni mdhamini    (wa  maamuma)”. Ibn Hibbaan

 

3. Kutenda kitendo kilichokatazwa  kwa  kusahau,  ikiwa  makusudi  yake   hubatilisha  swala. Mithili  ya mwenye kuswali kuzungumza maneno   machache au kuongeza rakaa moja kwa  kusahau.

Kisha akazinduka na kutambua  kuwa yumo ndani  ya swala, huyu katika  mazingira haya  ataleta  sijida mbili za  kusahau.

4. Kugurisha/kuhamisha kitu miongoni mwa  matendo ya swala kukipeleka mahala si  pake. Kikiwa kitu hicho ni nguzo/faradhi au  ni suna ya “Ba’adh”. 

Mfano wa haya  ni mtu  kusoma  Suuratil–Faatihah   (Al-hamdu) katika  kikao (mkao) cha Tashahudi badala  ya  mahala  pake ambapo ni katika Qiyaamu (kisimamo  cha   swala).

Au mtu kusoma Qunuut katika  rukuu badala ya mahala  pake ambapo ni  katika  Itidali ambayo huja baada ya kurukuu.  Au mtu kuisoma  sura ambayo ni suna, kuisoma  baada ya Al-hamdu katika Itidali badala ya  mahala pake  ambapo ni katika  Quyaamu.

Ni suna kwa mtu huyu kusujudu sijida mbili za kusahau mwishoni mwa swala yake  kutokana  na kuyafanya haya.

 

NAMNA  YA KUSUJUDU SIJIDA ZA KUSAHAU  NA MAHALA PA KUSUJUDU:

Kusujudu kwa kusahau   ni sijida mbili kama  sijida nyingine za swala. Mwenye  kuswali atanuia kwa sijida mbili hizo kusujudu  kwa kusahau.

Na mahala pa kusujudu ni  mwishoni mwa  swala yake  kabla ya  kutoa  salamu. Angalia  lau mwenye kuswali  atatoa salamu kabla ya  kusujudu kwa  makusudi  au  kwa kusahau na muda (kitambo) ukarepa  (ukarefuka), itafutu sijida  hiyo.

Kama  utakuwa  haukupita muda mrefu, itamuelea  kuidiriki  sijida  ya kusahau kwa kusujudu  mara mbili kwa nia ile ile ya kusahau,  kisha atoe salamu kwa mara nyingine tena.

 

TANBIHI:

1. Kama  mwenye   kuswali hakuleta sijida ya  kusahau ambayo hukumu yake  ni suna,  swala yake haitabatilika. Hii ni kwa  sababu  sijida ya kusahau  haikuwekwa  kwa ajili ya  kuacha tendo la wajibu.

2. Ama mwenye  kuswali atapoacha mojawapo ya  nguzo  za swala  kama rukuu au kusoma  Al-hamdu. Basi hana budi  kuileta nguzo hiyo aliyoiacha wala kusujudu kwa kusahau  hakutakuwa kiungo cha  nguzo hiyo. Bali  sijida mbili za kusahau zitakuja baada  ya  kuileta hiyo   nguzo  aliyoisahau.

 

SABABU ZA SIJIDA SAHW NA NAMNA YA KUISUJUDU

Mambo yafuatayo ndio yatakayo mpelekea mwenye kuswali  kuleta sijida ya  kusahau:

1. Mwenye kuswali kuacha  mojawapo  miongoni  mwa suna za swala zinazoitwa “Ab-aadh”, mithili ya Tashahudi ya mwanzo na Qunuut  (kwa ufafanuzi wa kina juu ya suna hizi, rejea SURA YA PILI, SOMO LA KWANZA, SWALA {x} Suna za swala).

Imepokewa kutoka kwa Abdullah Ibn Buhaynah-Allah amuwiye radhi–kwamba yeye amesema:  Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-alituswalisha rakaa mbili za  swala fulani.

(more…)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *