MAANA YA NAJISI

Najisi ni neno la kiarabu lenye maana mbili; maana ya kilugha na ya kisheria.

Najisi katika lugha ni kila kilicho kibaya hata kama ni twahara kama vile makamasi, makohozi, tongotongo na kadhalika. Maana hii ya najisi kilugha tunaipata katika kauli ya Mola anaposema :

“ENYI MLIOAMINI ! HAKIKA WASHIRIKINA NI NAJISI ….” [9:28]

Sote tunakubaliana kwa dalili zote; dalili nakala na dalili akili kwamba binadamu yeyote ni kiumbe twahara lakini utaona kwenye aya hii Mola Mtukufu anawaita washirikina kuwa ni NAJISI kwa sababu ya ubaya na uchafu wa nafsi zao katika katika kumshirikisha MwenyeziMungu na viumbe alivoviumba mwenyewe.

Kwa darubini ya sheria najisi ni kila kitu kichafu ambacho kinazuia kusihi kwa ibada kama vile swala, kutufu (twawafu) na kadhalika.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *