Mbona unashindwa kujiheshimu na kujistahi mwenyewe, basi japo waheshimu na wastahi watu wengine, kwa nini lakini uonyeshe uchi wako mbele za watu?! Kwa nini uvue nguo zako hata kabla ya kuingia maliwatoni?! Tambua hilo halifai na halipungui kuwa ni kumkhalifu aliye bora mno kuliko wewe; Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-kwani ni yeye: “Alikuwa anapo kwenda kukidhi haja, hasegi (hanyanyui juu) nguo zake, mpaka akurubie kwenye ardhi (mahala pa kukidhia haja”. Tirmidhiy [14] & Abu Daawpud [14]-Allah awarehemu.