| Makala |
| Uislamu-Utangulizi |
| Fiqhi
na Sheria |
| Akhlaaq-Tabia |
| Sira
ya Mtume |
| Nasaha
za dini |
| Maswali na Majibu
|
|
Uliza Suala la
dini |
|
Jiunge
!!! |
|
Minbari ya Ramadhani Swala ya
Tarawehe |
|
Tunaharakia kusema na tunawaambia maimamu wa Ijitihadi katika zama
hizi: Hakika aliyo yafanya Umar au aliyo yaamrisha Umar, si uzuzi
(bidaa) katika dini. Bali hilo ni kushikamana na muongozo wa Mtume
na ni kuifuata Sunna ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-kwa
sababu zifuatazo:
a) Kwamba Sayyidna Umar Bin
Al-Khatwaab, alipewa na Mtume jina la “Al-Faarouq”, kwa sababu Allah
aliifarikisha (aliitenganisha) haki na batili kupitia kwake. Na
alitenganisha kwaye uwongofu na upotofu, basi yeye ni Al-Faarouq
Umar-Allah amuwiye radhi.....Endelea |
|
| |
Karibu kwenye Mtandao wa
UISLAMU |
| |
|
"Soma kwa jina la Mola
wako Mlezi aliye
umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na
Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye
amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa
hayajui...." 96:1-5
|
|
|
|
|
|
|
| Dondoo za
wiki |
|
|
|
Hukumu za Eda
Ziko hukumu na lazima
zinazo wajibishwa na eda ambazo tunazibainisha
kama ifuatavyo:
Mosi: Eda ya talaka/kuachwa:
Atakapo kuwa mwanamke anamkalia eda
mume wake, eda ya kuachwa. Basi ama kuachwa
kwake huko kutakuwa ni talaka rejea au talaka
baini. Angalia:
(A)
Akiwa
anakaa eda kutokana na talaka rejea, eda yake
hiyo inaandamiwa na hukumu zifuatazo:
1.
Uwajibu
wa maskani (makazi) uko juu ya mume na lililo
bora ni kuwa yale yale maskani ya talaka yake
yakiwa yanachukuzana nae. Na hakuna kizuizi
chochote cha kisheria kinacho mzuia kukaa eda
humo na mfano wa hilo.
Endelea
....
|
|
Nguvu
Akida/itikadi iliyo kita moyoni, ni msaidizi
asiye ishiwa na utendaji endelevu na hamasa
zilizo hifadhiwa. Si hivyo tu, ni msaidizi mzuri
katika ulingo mzima wa kustahamilia magumu na
kuzikabili hatari. Tena ni dereva aendaye mbio
kukutana na mauti bila ya khofu. Hiyo ndio tabia
ya imani pale inapo penya, ikaingia na kukita
ndani ya mdau wake. Hakika imani ya namna hii,
humuundia mdau wake NGUVU inayo uathiri mwenendo
wake wote. Nguvu hii ndio inayo mfanya anapo
zungumza, kuwa mkweli wa kauli yake na anapo
fanya kazi hujikita vilivyo katika kazi hiyo. Na
anapo chukua muelekeo, basi huwa muwazi katika
malengo/shabaha zake. Na maadam ametulizana
kwenye fikra zinazo ijaza akili yake na zile
hisia zinazo ufunika moyo wake. Ni nadra mno
kusitasita na kutetereshwa na pepo zivumazo,
akauacha msimamo wa nafsi yake, tena si hivyo tu
lakini si jukumu lake kuwaambia wanao mzunguka
katika maisha yake ya kila siku: “...FANYENI
MWEZAVYO, MIMI PIA NAFANYA. BASI MTAKUJA ONA NI
NANI ITAKAYE MFIKIA ADHABU YA KUMHIZI, NA
ITAKAYE MSHUKIA ADHABU YA DAIMA”. [39:40] Endelea
.....
|
|
Ufunguzi wa Misri
Sayyidna Umar-Allah amuwiye radhi-katika kipindi cha ziara
yake ya Shamu, aliombwa na Amrou Bin Al-Aaswi
ruhusa ya kwenda kuifungua Misri. Na akamtajia
kheri zake na kwamba nchi hiyo ni nguvu kubwa ya
mamlaka ya Urumi na enzi hizo ilikuwa ni
mfuasi/mshirika wake. Ikitawaliwa na gavana
Mrumi aliye kuwa akiishi Iskandaria
(Alexandria). Sayyidna Umar akampeleka huko
Amrou na jeshi kubwa kama alivyo omba, baada ya
kuondoka akampelekea kikosi kingine chini ya
Zubeir Bin Al-Awwaam. Wote kwa pamoja wakaingia
kwa kupitia mlango wa Alyoun, wakapita kwenye
vijiji vya mshambani mpaka wakatokea Misri.
Endelea ...
|
Mazungumzo juu ya
upweke wa Allah ...Inaendelea
TANO: Kukimbia kabisa kumshirikisha Allah
Ataadhamiaye, kukimbia kutakako mfanya mtu
timamu wa akili kuiweka mbali nafsi yake dhidi
ya kuikurubia shirki. Na ukimbiaji huu umekuja
kwa mitindo aina kwa aina.
Miongoni mwa mitindo hiyo: Ni
kufumbuliza ya kwamba Allah Atukukiaye anasemehe
dhambi zote isipo kuwa shirki. Allah
Ataadhamiaye amesema: “HAKIKA ALLAH HASAMEHI
KUSHIRIKISHWA, NA HUSAMEHE YALIYO DUNI YA HILO
KWA AMTAKAYE. NA ANAYE MSHIRIKISHA ALLAH BASI
HAKIKA AMEZUA DHAMBI KUBWA”. [04:48] Endelea ... | |
|
| |
|
|
|
| Aya ya Wiki |
|
“NA KATIKA WATU YUKO AMBAYE
HUIUZA NAFSI YAKE KWA KUTAKA RADHI ZA ALLAH; NA
ALLAH NI MPOLE KWA WAJA WAKE”. [02:207]
|
|
| Hadith ya Wiki |
|
Mtume wa Allah-Rehema na Amani
zimshukie-amesema: “Kumempasa kila muislamu
kutoa sadaka, wakauliza: Ewe Nabii wa Allah!
Unaonaje kama hakupata? Akajibu: Afanye kazi kwa
mkono wake, ajinufaishe yeye na atoe sadaka.
Wakauliza: Je, kama hakuweza (huko kufanya
kazi)? Akajibu: Amsaidie mwenye shida, mwenye
simanzi. Wakauliza: Je, kama hakupata (cha
kumsaidia)? Akajibu: Basi na aamrishe wema.
Wakauliza: Je, kama hakufanya hivyo? Akajibu:
Basi na ajizuie na kutenda shari/maovu, kwani
hilo ni sadaka”. Bukhaariy-Allah amrehemu.
|
|
| Katazo
la Wiki |
|
Ni kweli kuwa hakuna mtu asiye
patwa na shida/haja. Nduguyo amekwama, hana kitu
na hivyo kulazimika kuja kukopa kwa nia ya
kukulipa pindi mambo yake yatakapo kaa sawa.
Sasa hajapata, na wewe hujasongeka hivyo, kwa
nini basi umnyime raha kwa kumdai kwa karaha?!
Acha huo sio Uislamu, kwani wewe huiamini kauli
hii ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie:
“Atakaye msubiria asiye na kitu au akampomoshea
deni, Allah atamuweka chini ya kivuli cha Arshi
katika siku ambayo hapatakuwa na kivuli ila
kivuli cha Arshi yake tu”. Ahmad-Allah amrehemu.
|
|
Swali
la Wiki |
|
SWALI: Nini hukumu ya kununua
hisa katika mashirika ya kibiashara ambayo
yanaendeshwa kwa mtindo wa riba?
JIBU: Walionalo Wanachuoni, ni
kwamba ucha-Mngu ni kuacha kununua hisa katika
mashirika kama hayo na kukaa mbali nayo kabisa.
Kwa sababu ghalibu ya mashirika hayo huendeshwa
kwa misingi ya riba, na Mtume wa Allah-Rehema na
Amani zimshukie-amekwisha sema: “Acha ulilo na
mashaka nalo na tenda usilo na shaka nalo”.
Tirmidhiy [2518] & Nasaai [5711]-Allah
awarehemu.
Na amesema: “Atakaye jiepusha na
mambo yenye shubuha, bila ya shaka huyo
ameihifadhi dini yake na heshima yake”.
bukhaariy [52] & Muslim [1599]-Allah awarehemu.
Allah ndiye Mjuzi mno.
|
|
| |
|
| Tuandikie |
| |
|
|
![]() |
|