Last Update :  30 Agosti 2010 (Jumatatu)
   19 Ramadhani  1431 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!
Minbari ya Ramadhani Swala ya Tarawehe

Tunaharakia kusema na tunawaambia maimamu wa Ijitihadi katika zama hizi: Hakika aliyo yafanya Umar au aliyo yaamrisha Umar, si uzuzi (bidaa) katika dini. Bali hilo ni kushikamana na muongozo wa Mtume na ni kuifuata Sunna ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-kwa sababu zifuatazo:
a)
Kwamba Sayyidna Umar Bin Al-Khatwaab, alipewa na Mtume jina la “Al-Faarouq”, kwa sababu Allah aliifarikisha (aliitenganisha) haki na batili kupitia kwake. Na alitenganisha kwaye uwongofu na upotofu, basi yeye ni Al-Faarouq Umar-Allah amuwiye radhi.....Endelea

  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5


Dondoo za wiki

Hukumu za Eda
        Ziko hukumu na lazima zinazo wajibishwa na eda ambazo tunazibainisha kama ifuatavyo:
Mosi: Eda ya talaka/kuachwa:

         Atakapo kuwa mwanamke anamkalia eda mume wake, eda ya kuachwa. Basi ama kuachwa kwake huko kutakuwa ni talaka rejea au talaka baini. Angalia:
               
(A)         
Akiwa anakaa eda kutokana na talaka rejea, eda yake hiyo inaandamiwa na hukumu zifuatazo:
                                         
1.         
Uwajibu wa maskani (makazi) uko juu ya mume na lililo bora ni kuwa yale yale maskani ya talaka yake yakiwa yanachukuzana nae. Na hakuna kizuizi chochote cha kisheria kinacho mzuia kukaa eda humo na mfano wa hilo. Endelea ....


Nguvu 
Akida/itikadi iliyo kita moyoni, ni msaidizi asiye ishiwa na utendaji endelevu na hamasa zilizo hifadhiwa. Si hivyo tu, ni msaidizi mzuri katika ulingo mzima wa kustahamilia magumu na kuzikabili hatari. Tena ni dereva aendaye mbio kukutana na mauti bila ya khofu. Hiyo ndio tabia ya imani pale inapo penya, ikaingia na kukita ndani ya mdau wake. Hakika imani ya namna hii, humuundia mdau wake NGUVU inayo uathiri mwenendo wake wote. Nguvu hii ndio inayo mfanya anapo zungumza, kuwa mkweli wa kauli yake na anapo fanya kazi hujikita vilivyo katika kazi hiyo. Na anapo chukua muelekeo, basi huwa muwazi katika malengo/shabaha zake. Na maadam ametulizana kwenye fikra zinazo ijaza akili yake na zile hisia zinazo ufunika moyo wake. Ni nadra mno kusitasita na kutetereshwa na pepo zivumazo, akauacha msimamo wa nafsi yake, tena si hivyo tu lakini si jukumu lake kuwaambia wanao mzunguka katika maisha yake ya kila siku: “...FANYENI MWEZAVYO, MIMI PIA NAFANYA. BASI MTAKUJA ONA NI NANI ITAKAYE MFIKIA ADHABU YA KUMHIZI, NA ITAKAYE MSHUKIA ADHABU YA DAIMA”. [39:40] 
Endelea .....


Ufunguzi wa Misri
Sayyidna Umar-Allah amuwiye radhi-katika kipindi cha ziara yake ya Shamu, aliombwa na Amrou Bin Al-Aaswi ruhusa ya kwenda kuifungua Misri. Na akamtajia kheri zake na kwamba nchi hiyo ni nguvu kubwa ya mamlaka ya Urumi na enzi hizo ilikuwa ni mfuasi/mshirika wake. Ikitawaliwa na gavana Mrumi aliye kuwa akiishi Iskandaria (Alexandria). Sayyidna Umar akampeleka huko Amrou na jeshi kubwa kama alivyo omba, baada ya kuondoka akampelekea kikosi kingine chini ya Zubeir Bin Al-Awwaam. Wote kwa pamoja wakaingia kwa kupitia mlango wa Alyoun, wakapita kwenye vijiji vya mshambani mpaka wakatokea Misri.    Endelea ...


Mazungumzo juu ya upweke wa Allah ...Inaendelea
TANO: Kukimbia kabisa kumshirikisha Allah Ataadhamiaye, kukimbia kutakako mfanya mtu timamu wa akili kuiweka mbali nafsi yake dhidi ya kuikurubia shirki. Na ukimbiaji huu umekuja kwa mitindo aina kwa aina.

Miongoni mwa mitindo hiyo: Ni kufumbuliza ya kwamba Allah Atukukiaye anasemehe dhambi zote isipo kuwa shirki. Allah Ataadhamiaye amesema: “HAKIKA ALLAH HASAMEHI KUSHIRIKISHWA, NA HUSAMEHE YALIYO DUNI YA HILO KWA AMTAKAYE. NA ANAYE MSHIRIKISHA ALLAH BASI HAKIKA AMEZUA DHAMBI KUBWA”. [04:48]  Endelea ...

 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“NA KATIKA WATU YUKO AMBAYE HUIUZA NAFSI YAKE KWA KUTAKA RADHI ZA ALLAH; NA ALLAH NI MPOLE KWA WAJA WAKE”. [02:207]

 

Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Kumempasa kila muislamu kutoa sadaka, wakauliza: Ewe Nabii wa Allah! Unaonaje kama hakupata? Akajibu: Afanye kazi kwa mkono wake, ajinufaishe yeye na atoe sadaka. Wakauliza: Je, kama hakuweza (huko kufanya kazi)? Akajibu: Amsaidie mwenye shida, mwenye simanzi. Wakauliza: Je, kama hakupata (cha kumsaidia)? Akajibu: Basi na aamrishe wema. Wakauliza: Je, kama hakufanya hivyo? Akajibu: Basi na ajizuie na kutenda shari/maovu, kwani hilo ni sadaka”. Bukhaariy-Allah amrehemu.

 

Katazo la Wiki

Ni kweli kuwa hakuna mtu asiye patwa na shida/haja. Nduguyo amekwama, hana kitu na hivyo kulazimika kuja kukopa kwa nia ya kukulipa pindi mambo yake yatakapo kaa sawa. Sasa hajapata, na wewe hujasongeka hivyo, kwa nini basi umnyime raha kwa kumdai kwa karaha?! Acha huo sio Uislamu, kwani wewe huiamini kauli hii ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie: “Atakaye msubiria asiye na kitu au akampomoshea deni, Allah atamuweka chini ya kivuli cha Arshi katika siku ambayo hapatakuwa na kivuli ila kivuli cha Arshi yake tu”. Ahmad-Allah amrehemu.

 

Swali la Wiki

SWALI: Nini hukumu ya kununua hisa katika mashirika ya kibiashara ambayo yanaendeshwa kwa mtindo wa riba?

 

JIBU: Walionalo Wanachuoni, ni kwamba ucha-Mngu ni kuacha kununua hisa katika mashirika kama hayo na kukaa mbali nayo kabisa. Kwa sababu ghalibu ya mashirika hayo huendeshwa kwa misingi ya riba, na Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amekwisha sema: “Acha ulilo na mashaka nalo na tenda usilo na shaka nalo”. Tirmidhiy [2518] & Nasaai [5711]-Allah awarehemu.

Na amesema: “Atakaye jiepusha na mambo yenye shubuha, bila ya shaka huyo ameihifadhi dini yake na heshima yake”. bukhaariy [52] & Muslim [1599]-Allah awarehemu.

Allah ndiye Mjuzi mno.

 


| Tuandikie |

: