|
SWALI: Baadhi ya wafanya
biashara ya nguo, huwauzia mabinti wadogo mavazi
mafupi, yanayo acha wazi maungo yao. Je, uuzaji
huu unaingia katika wigo wa kusaidiana katika
dhambi na uadui, kulikotajwa na Allah katika
aya?
JIBU: Bila ya shaka, kuuza
kilicho harimishwa ni HARAMU kwa mujibu wa kauli
ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie:
“Hakika Allah anapo harimisha kitu chochote,
imeharimika na thamani yake (kitu hicho)”. Abu
Daawoud [3488] & Ahmad [01/322, 293, 247]-Allah
awarehemu.
Allah ndiye Mjuzi mno. |