Last Update :  3 Februari 2010 (Jumatano)
   19 Safar (Mfungo tano)  1431 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!
 
 
  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5


Dondoo za wiki

Namna zilizoshariiwa talaka
Kunamkinika kutusha (kutoa) talaka kwa namna mbali mbali, kama vile kuzichanganya pamoja talaka tatu kwa tamko moja au kwa kutenganisha baina yake. Au kuitusha talaka tinda; isiyo na sharti au yenye kuangikwa juu ya sharti fulani au pamoja na kuvua. Endelea ....


Utakasifu wa nia (Ikhlaasi)
Hakika vipelekeshi/misukumo ambayo inayo mpelekea mtu kutenda amali na kumsukuma kuitenda vema amali hiyo. Na kumuhimiza kuchukua/kustahamili taabu katika njia ya kuitenda amali hiyo au kutoa vingi ili kuifikia. Vipelekeshi/misukumo hiyo ni mingi na ni yenye kutofautiana. Miongoni mwake, iko ile ambayo ni ya karibu, inayo karibia kuonekana pamoja na amali tendwa. Na iko ambayo hiyo ni yenye kufichikana ndani kabisa ya uvungu wa moyo wa mtenda amali hiyo. Na wakati mwingine huenda hata asiidiriki (asiitambue) hata huyo mtenda amali mwenyewe aliye athiriwa nayo. Pamoja na kwamba kihakika hasa hiyo ndiyo siri iliyo mfanya ajitome kutenda alilo litenda au kuacha alilo liacha kulitenda. 
Endelea .....


Hurmuzaan abatilisha mipaka iliyowekwa  
Baada ya suluhu na kuandikwa kwa mkataba wa amani baina ya mshindwa; Hurmuzaan na washindi Waislamu kwa masharti yaliyo wekwa na Waislamu. Hurmuzaan aliacha kuendelea kuuheshimu mkataba huo, kwa sababu ya kutokuelewana katika uwekwaji wa mipaka kuliko tokea baina yake na  wale walinzi wa ngome ya Manaadhir na ile ya mto Tairi. Hurmuzaan akaomba msaada kwa Wakurdi, wamsaidie kumaliza udhia wa Waislamu. Gavana wa Basra; Utbah akamwandikia waraka Amirul-Muuminina kumfahamisha hali ya mambo ilivyo, ili kupata maelekezo ya nini cha kufanya kutoka kwake. Sayyidna Umar akampa Utbah idhini ya kwenda kukabiliana na mpinzani/muasi huyu.  Endelea ...


Usawa katika haki za Jamii  
Bila ya shaka, mwenye kuizingatia sheria ya Uislamu, ataiona imeweka usawa baina ya wanaume na wanawake katika kile kinacho julikana kama “haki za kijamii” kwa aina zake zote. Hizi ni kama vile haki ya kununua na kuuza, haki ya kumiliki mali, haki ya kutumia kilicho katika milki, haki ya uwakala na baki ya hizo. Na miongoni mwa dalili/ushahidi wa hili, ni kama ifuatavyo: 
 Endelea ...

 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“ENYI WATU! IKIWA NYINYI MNA SHAKA YA KUFUFULIWA, BASI KWA HAKIKA SISI TULIKUUMBENI KWA UDONGO, KISHA KUTOKANA NA MANII, KISHA KUTOKANA NA KIPANDE CHA DAMU ILIO GANDANA, KISHA KUTOKANA NA KIPANDE CHA NYAMA CHENYE UMBO NA KISICHO KUWA NA UMBO, ILI TUKUBAINISHIENI. NASI TUNAKIWEKA KATIKA MATUMBO YA UZAZI TUNACHO KITAKA MPAKA MUDA ULIO WEKWA. KISHA MFIKIE KUTIMIA AKILI. NA WAPO KATIKA NYINYI WANAO KUFA, NA WAPO KATIKA NYINYI WANAO RUDISHWA KWENYE UMRI WA UNYONGE KABISA, HATA MTU AWE HAJUI KITU BAADA YA KUWA ANAKIJUA...” [22:05]

Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Salama ya mtu katika (hali/wakati wa) fitina ni kulazimikiana na nyumba yake”. Dailamiy-Allah amrehemu.

Katazo la Wiki

Uongozi ni amana na dhima kutoka kwa Allah na kwa upande wa pili ni makujumu kwa waja wa Allah. Allah amekuteua na watu wamekuchagua uwaongoze. Kwa nini basi unaikhini amana hii ya Allah na kuyatupa majukumu ya waja wa Allah kwa kutokuwa muadilifu kwa raia wako?! Angalia, usije kuikosa pepo ya Allah: “Hapana kiongozi yeyote anaye watawalia raia katika Waislamu, basi akafa ilhali anawafanyia ghushi ila Allah atamuharimishia pepo”. Bukhaariy & Muslim-Allah awarehemu.

Swali la Wiki

SWALI: Baadhi ya wafanya biashara ya nguo, huwauzia mabinti wadogo mavazi mafupi, yanayo acha wazi maungo yao. Je, uuzaji huu unaingia katika wigo wa kusaidiana katika dhambi na uadui, kulikotajwa na Allah katika aya?

 

JIBU: Bila ya shaka, kuuza kilicho harimishwa ni HARAMU kwa mujibu wa kauli ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie: “Hakika Allah anapo harimisha kitu chochote, imeharimika na thamani yake (kitu hicho)”. Abu Daawoud [3488] & Ahmad [01/322, 293, 247]-Allah awarehemu.

Allah ndiye Mjuzi mno.


| Tuandikie |

: