|
| Dondoo za
wiki |
|
|
|
Hekima ya kuwekwa sharia yaMirathi Hakika
katika kuwekwa kwa sharia ya mirathi na ugavi wa tarika ya maiti baina
ya warithi wake, zipo hekima nyingi zilizo wazi, tunazitaja baadhi yake
kama ifuatavyo:
1. Kuliridhisha umbile finyango la mwanaadamu, kwani
hakika Allah amemuumba mwanaadamu na akaumba ndani yake mapenzi ya
kupata/kuwa na mtoto. Mtoto ambaye anaona pambo la maisha ndani yake,
uendelevu wa maisha yake na kielelezo cha kusalia utajo wake baada ya
kufariki kwake. Ni kwa ajili/sababu hiyo basi, hujipinda na kutaabika
kwa ajili ya mwanawe. Na kwa kupitia jitihada na utendaji huo, maisha
huchanua na kukithiri kheri ndani yake. Na lau dini ingeli harimisha
mirathi/kurithiana baina ya mtu na mtu au baina ya kizazi na kizazi,
basi ingeli dorora raghba na ari ya kufanya kazi na kuustawisha
ulimwengu katika uwepo wa wana wa Adamu. Endelea
....
|
|
Kuchagua marafiki
...inaendelea
Uislamu unamuacha muumini awe mahala ambapo panapo mea
heshima binafsi/hadhi/utukufu na unamtunukia uhuru kamili unao
komelea pale inapo anzia haki ya mtu mwingine. Kwa hivyo basi, ni
wajibu wa muumini huyo kuhakikisha kuwa anaishi na maana hiyo katika
mazingira yake yanayo mzunguka, katika kila hatua na kipengele cha
maisha yake ya kila uchao. Na akishindwa kulipata hilo hapo alipo,
basi na agure kutoka katika nyumba/mji/nchi hiyo ya udhalili,
akaitafute hadhi/heshima/utu kule unako patikana, kokote kule kuwako
katika ardhi ya Allah; Mola Muumba wake.
.Endelea
.....
|
|
Vita vya Swaffein Bwana Muawiya alipo litambua hilo, ya kwamba Amirul-Muuminina;
Sayyidna Aliy-Allah amuwiye radhi-ametoka na jeshi lake kuja
kupambana naye, naye akatoka kumfuata akiyaongoza majeshi ya Shamu.
Majeshi mawili; jeshi la Imamu Aliy na lile la Muawiya, yakakutana
kwenye tambarare za Swaffein, zilizoko kando kando ya mto Furaati,
Mashariki mwa mji wa Halbi. Majeshi yakapiga kambi kwa muda wa siku
mbili, ambapo baada yake pande mbili hizo zikaanza kupelekeana
wajumbe wa amani, ili kujaribu kuepusha umwagaji wa damu za Waislamu
wenyewe kwa wenyewe.
Endelea ...
|
Majadiliano na
watu wa Kitabu...Inaendelea
Ndugu msomaji wetu nwema-Allah akurehemu-bila ya shaka wewe kupitia
mazungumzo/majadiliano haya, ambayo Allah Ataadhamiaye alimuamrisha
Mtume wake-Rehema na Amani zimshukie. Kuwarudi kwao Mayahudi ambao
walio dai kwamba wao wanayaamini waliyo teremshiwa. Awarudi kwa
marejezo yatakayo batilisha madai hayo kwa nyajihi kadhaa, nazo ni:
Kuwauwa kwao mitume, kuabudu kwao kigombe, kuvunja kwao ahadi na
maagano na kumwambia kwao yule aliye wanasihi, tumeyasikia maneno
yako na tumeikataa amri yako. Na mambo mabaya haya yanakatazwa na
Taurati ambayo wao wanadai kuiamini hiyo tu. Endelea ...
| |
|
| |
|
|
|
| Aya ya Wiki |
|
“JE! HUONI KWAMBA VINAMSUJUDIA ALLAH VILIOMO MBINGUNI NA VILIOMO
KATIKA ARDHI, NA JUA, NA MWEZI, NA NYOTA, NA MILIMA, NA MITI, NA
WANYAMA, NA WENGI MIONGONI MWA WATU. NA WENGI IMEWASTAHIKI ADHABU. NA
ANAYE FEDHEHESHWA NA ALLAH HANA WA KUMHISHIMU. HAKIKA ALLAH HUTENDA
APENDAVYO”. [22:18]
|
|
| Hadith ya Wiki |
|
Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Hayachanganyiki
mahaba yangu na moyo wa mja, ila Allah atakiharimisha kiwiliwili
chake na moto”. Abu Nuaim-Allah amrehemu.
|
|
| Katazo
la Wiki |
|
Kwa nini lakini, ugeuke na kuwa ni kero/maudhi kwa jirani zako?! Kwa
nini wewe ndio uwe chanzo/sababu ya maafa na usumbufu kwa jirani zako
kiasi cha wao kutamani kuwa mbali nawe?! Tahadhari, kwani Mtume wa
Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesha sema: “Wallah haamini
(haikamiliki imani yake), wallah haamini, wallah haamini! Pakaulizwa:
Ni nani huyo ewe Mtume wa Allah? Akajibu: Yule ambaye jirani yake
hasalimiki na shari zake”. Bukhaariy-Allah amrehemu.
|
|
Swali
la Wiki |
|
SWALI: Je, kutayamamu kwa ajili ya swala kunawalazimu wanawake kama
kunavyo walazimu wanaume au kumewakhusu wanaume peke yao katika hali
ya kukosekana kwa maji?
JIBU: Lililo asili/msingi katika hukumu ni uenevu kwa wote wanaume na
wanawake, ila ile hukumu ambayo kumekuja ndani yake kuvuliwa kwa
mmoja wao, haya ni kwa mujibu wa kauli yake Allah Ataadhamiaye: “ENYI
MLIO AMINI! MNAPO SIMAMA KWA AJILI YA SWALA BASI OSHENI NYUSO ZENU,
NA MIKONO YENU MPAKA VIFUNDONI, NA MPAKE VICHWA VYENU, NA OSHENI
MIGUU YENU MPAKA VIFUNDONI. NA MKIWA NA JANABA BASI OGENI. NA MKIWA
WAGONJWA AU MMO SAFARINI, AU MMOJA WENU AMETOKA CHOONI AU MMEWAGUSA
WANAWAKE, NA HAMKUPATA MAJI, BASI TAYAMAMUNI VUMBI LILILO SAFI, NA
MPAKE NYUSO ZENU NA MIKONO YENU. HAPENDI ALLAH KUKUTIENI KATIKA
TAABU; BALI ANATAKA KUKUTAKASENI NA KUTIMIZA NEEMA YAKE JUU YENU ILI
MPATE KUSHUKURU”. [05:06]
Amri ya kutayamamu katika aya hii inawaenea wote; wanaume na wanawake
nao wako sawa katika hukumu yao.
Allah ndiye Mjuzi mno.
|
|
|