Last Update :  13 Februari 2013 (Jumatano)
   3 Rabiul-Thani (Mfungo Saba) 1434 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!


  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5








Dondoo za wiki

Hekima ya kuwekwa sharia yaMirathi
 Hakika katika kuwekwa kwa sharia ya mirathi na ugavi wa tarika ya maiti baina ya warithi wake, zipo hekima nyingi zilizo wazi, tunazitaja baadhi yake kama ifuatavyo:
   1. Kuliridhisha umbile finyango la mwanaadamu, kwani hakika Allah amemuumba mwanaadamu na akaumba ndani yake mapenzi ya kupata/kuwa na mtoto. Mtoto ambaye anaona pambo la maisha ndani yake, uendelevu wa maisha yake na kielelezo cha kusalia utajo wake baada ya kufariki kwake. Ni kwa ajili/sababu hiyo basi, hujipinda na kutaabika kwa ajili ya mwanawe. Na kwa kupitia jitihada na utendaji huo, maisha huchanua na kukithiri kheri ndani yake. Na lau dini ingeli harimisha mirathi/kurithiana baina ya mtu na mtu au baina ya kizazi na kizazi, basi ingeli dorora raghba na ari ya kufanya kazi na kuustawisha ulimwengu katika uwepo wa wana wa Adamu. Endelea ....


Kuchagua marafiki ...inaendelea 
Uislamu unamuacha muumini awe mahala ambapo panapo mea heshima binafsi/hadhi/utukufu na unamtunukia uhuru kamili unao komelea pale inapo anzia haki ya mtu mwingine. Kwa hivyo basi, ni wajibu wa muumini huyo kuhakikisha kuwa anaishi na maana hiyo katika mazingira yake yanayo mzunguka, katika kila hatua na kipengele cha maisha yake ya kila uchao. Na akishindwa kulipata hilo hapo alipo, basi na agure kutoka katika nyumba/mji/nchi hiyo ya udhalili, akaitafute hadhi/heshima/utu kule unako patikana, kokote kule kuwako katika ardhi ya Allah; Mola Muumba wake.

.Endelea .....


Vita vya Swaffein
Bwana Muawiya alipo litambua hilo, ya kwamba Amirul-Muuminina; Sayyidna Aliy-Allah amuwiye radhi-ametoka na jeshi lake kuja kupambana naye, naye akatoka kumfuata akiyaongoza majeshi ya Shamu. Majeshi mawili; jeshi la Imamu Aliy na lile la Muawiya, yakakutana kwenye tambarare za Swaffein, zilizoko kando kando ya mto Furaati, Mashariki mwa mji wa Halbi. Majeshi yakapiga kambi kwa muda wa siku mbili, ambapo baada yake pande mbili hizo zikaanza kupelekeana wajumbe wa amani, ili kujaribu kuepusha umwagaji wa damu za Waislamu wenyewe kwa wenyewe.    Endelea ...


Majadiliano na watu wa Kitabu...Inaendelea
Ndugu msomaji wetu nwema-Allah akurehemu-bila ya shaka wewe kupitia mazungumzo/majadiliano haya, ambayo Allah Ataadhamiaye alimuamrisha Mtume wake-Rehema na Amani zimshukie. Kuwarudi kwao Mayahudi ambao walio dai kwamba wao wanayaamini waliyo teremshiwa. Awarudi kwa marejezo yatakayo batilisha madai hayo kwa nyajihi kadhaa, nazo ni: Kuwauwa kwao mitume, kuabudu kwao kigombe, kuvunja kwao ahadi na maagano na kumwambia kwao yule aliye wanasihi, tumeyasikia maneno yako na tumeikataa amri yako. Na mambo mabaya haya yanakatazwa na Taurati ambayo wao wanadai kuiamini hiyo tu.

 Endelea ...


 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“JE! HUONI KWAMBA VINAMSUJUDIA ALLAH VILIOMO MBINGUNI NA VILIOMO KATIKA ARDHI, NA JUA, NA MWEZI, NA NYOTA, NA MILIMA, NA MITI, NA WANYAMA, NA WENGI MIONGONI MWA WATU. NA WENGI IMEWASTAHIKI ADHABU. NA ANAYE FEDHEHESHWA NA ALLAH HANA WA KUMHISHIMU. HAKIKA ALLAH HUTENDA APENDAVYO”. [22:18]



Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Hayachanganyiki mahaba yangu na moyo wa mja, ila Allah atakiharimisha kiwiliwili chake na moto”. Abu Nuaim-Allah amrehemu.

 


Katazo la Wiki

Kwa nini lakini, ugeuke na kuwa ni kero/maudhi kwa jirani zako?! Kwa nini wewe ndio uwe chanzo/sababu ya maafa na usumbufu kwa jirani zako kiasi cha wao kutamani kuwa mbali nawe?! Tahadhari, kwani Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesha sema: “Wallah haamini (haikamiliki imani yake), wallah haamini, wallah haamini! Pakaulizwa: Ni nani huyo ewe Mtume wa Allah? Akajibu: Yule ambaye jirani yake hasalimiki na shari zake”. Bukhaariy-Allah amrehemu.

 

Swali la Wiki

SWALI: Je, kutayamamu kwa ajili ya swala kunawalazimu wanawake kama kunavyo walazimu wanaume au kumewakhusu wanaume peke yao katika hali ya kukosekana kwa maji?

JIBU: Lililo asili/msingi katika hukumu ni uenevu kwa wote wanaume na wanawake, ila ile hukumu ambayo kumekuja ndani yake kuvuliwa kwa mmoja wao, haya ni kwa mujibu wa kauli yake Allah Ataadhamiaye: “ENYI MLIO AMINI! MNAPO SIMAMA KWA AJILI YA SWALA BASI OSHENI NYUSO ZENU, NA MIKONO YENU MPAKA VIFUNDONI, NA MPAKE VICHWA VYENU, NA OSHENI MIGUU YENU MPAKA VIFUNDONI. NA MKIWA NA JANABA BASI OGENI. NA MKIWA WAGONJWA AU MMO SAFARINI, AU MMOJA WENU AMETOKA CHOONI AU MMEWAGUSA WANAWAKE, NA HAMKUPATA MAJI, BASI TAYAMAMUNI VUMBI LILILO SAFI, NA MPAKE NYUSO ZENU NA MIKONO YENU. HAPENDI ALLAH KUKUTIENI KATIKA TAABU; BALI ANATAKA KUKUTAKASENI NA KUTIMIZA NEEMA YAKE JUU YENU ILI MPATE KUSHUKURU”. [05:06]

Amri ya kutayamamu katika aya hii inawaenea wote; wanaume na wanawake nao wako sawa katika hukumu yao.

Allah ndiye Mjuzi mno.

 



| Tuandikie |



: